STAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel na shostito wake Nice Chande, juzikati walijikuta walitifuana kwa matusi makali ya nguoni nyumbani kwa rafiki yao Wema Sepetu ‘Madam’ anayeishi mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Wakiwa na dalili zote za kubugia kiburudisho cha kutosha kilichowafanya wasione vibaya kupaza sauti za matusi mbele za watu, marafiki hao walitoka ndani ya nyumba hiyo na kuendelea kutukanana kana kwamba hawana akili nzuri.
Kuona hivyo, watatu hao walishuka na kuanza kurudi tena nyumbani kwa Wema, ambaye aliendelea kuwasihi lakini wakiendelea kushambulia kwa maneno makali, kila mmoja akimlaumu mwenzake kuwa ndiye chanzo cha ajali ile.
Nyumbani kwa Wema, wasanii hao walimuomba msaidizi wake, Petit Man aende kuwasaidia kulinasua gari hilo mtaroni, kazi ambayo ilifanywa na vijana wa mtaani hapo waliolipwa kiasi cha shilingi 50,000.
Hata hivyo, baada ya gari hili kuletwa kwa Wema, si Aunt wala Nice waliokuwa tayari kulipanda, hali iliyomlazimisha mwenyeji wao kupiga simu kuita teksi, ambayo pia baada ya kufika, Nice alikataa kuipanda, badala yake Aunt na shostito wao mwingine ndiyo waliingia ndani na kutokomea.
Baada ya kukubaliana kuwa gari lile lilale hapo, Wema alimtaka Nice kuingia ndani, lakini aligoma, akidai anataka kuongea na baby wake kwa njia ya simu, lakini mwenyeji wake aliamua kuita teksi nyingine ambayo ilifika na kumchukua.
0 comments:
Post a Comment