Sunday, August 31, 2014

Aibu Kubwa Kwa Lulu Michael, Mke Wa Kigogo Afunguka Na Aonyesha Meseji Za Ngono Alizokuwa Anatuma Lulu Kwenda Kwa Mume Wake, Tazama hapa


Ni muda mrefu nimekuwa nikifuatilia mienendo ya mume wangu kutokana na tabia yake kubadilika sana siku za hivi karibuni, nikabaini kuwa kuna msichana anawasiliana naye kwa kutumiana meseji za mapenzi, sikuwa na haraka nikaamua kufanya uchunguzi wangu kimyakimya”
“Wiki iliyopita mume wangu akiwa amekwenda kuoga akasahau kuzima simu yake,na siyo kawaida yake kuacha simu yake bila kuizima,mara meseji ikaingia,nikaangalia nikaona jina la mtumaji amesevu Lulu, moyo ukalipuka”
Ndivyo alivyoanza kuongea mama mmoja wa makamo anayefanyakazi katika ofisi moja nyeti katikati ya jiji la Dar alipokuja kuongea na mwandishi wetu wiki iliyopita baada ya ndoa yake kuingiliwa na mdudu mbaya….

Akiongea kwa masikitiko makubwa, mama huyo ambaye hakupenda kutaja jina lake kutokana na unyeti wa kazi anayoifanya, alidai kuwa msichana huyo anayetaka kuiharibu ndoa yake yenye miaka 25 jina lake ni Elizabeth Michael….

Mama  huyo  alidai  kuwa  jina  hilo  alilibaini  baada  ya  kukuta  meseji  za  mapenzi  kwenye  simu  ya  mume  wake  na  yeye  kuamua  kuifuatilia  namba  hiyo  kwa  kufanya  kama  anataka  kumtumia  pesa  msichana  huyo  na  kukugundua  jina  hilo….
Akiongea  kwa  upole, mama  huyo  alidai  kuwa katika  simu  ya  mume  wake, jina  la  mtumaji  lilikuwa  Lulu, lakini  alipofanya  uchunguzi  wake  wa  kujifanya  kama anatuma  pesa  kwa  namba  ya  msichana  huyo  ndipo  alipobaini  kuwa  mmiliki  wa  namba  hiyo  ni  Elizabeth  Michael…
Mwandishi  alimuuliza  mama  huyo  kama  anadhani  kuwa  msichana  huyo  anayetaka  kuiharibu  ndoa  yake  ni  muigizaji  maarufu  wa  filamu  hapa  nchini Elizabeth  Michael  “Lulu”, lakini  alikataa  kuthibitisha  hilo  kwa  madai  kuwa  tangu  siku  hiyo  namba  ya  binti  huyo  imekuwa  haipatikani….
“Baada  ya  kugundua  siku  ile ,  nilichukua  simu  yake  na  kutaka  kuwasiliana  naye  ili  niweze  kumuonya  mwenyewe  kimyakimya  kwa  wakati  wangu, wala  sikuwa  na  lengo  la  kuja  kwenye  vyombi  vya  habari , lakini  sikuwahi  kumpata  hewani  tena  kila  nilipojaribu  kumpigia”Alisema  na  kuongeza:
“Huenda  mume  wangu  alishtikia  kuwa  nimeona  ujumbe  ule, kwa  sababu  mimi  nilipoisoma  meseji  ile  sikuifuta, ili  akiona  meseji  imesomwa  aelewe  nimeshajua  kila  kitu, pengine  ndiye  aliyemwambia  binti  huyo  abadili  namba  yake”
Mwandishi  alimuomba  mama  huyo  ampatie  namba  ya  huyo  msichana  ili  kuweza  kujua  kama  ni  Lulu  muigizaji  ama  siyo ( mwandishi  anazijua  namba  zote  za  Lulu ), lakini  namba  hiyo  ni  tofauti  na  anazotumia  Lulu  Mwenyewe….
Mwandishi  alipojaribu  kama  kumtumia  pesa  msichana  huyo, jina  lililotokeza  ni  Elizabeth Michael, na  alipojaribu  kuipiga  namba  hiyo  ilikuwa  haipatikani  hewani….
Juhudi  za  kumsaka  Lulu   ili  kuona  kama  anaitambua  namba  hiyo  hazikuzaa  matunda  kutokana  na  namba  zake  mbili  kutopatikana  na  nyingine  ikiita  bila  kupokelewa….
Angalizo:

Baadhi  ya  wasichana  wa  mjini  wamekuwa  wakitumia  majina  ya  wasanii  maarufu  katika  nyendo  zao  ili  kuwatapeli  watu. Miongoni  mwa  njia  wanazotumia  ni  pamoja  na   kujisajili  kwenye  mitandao  ya  kijamii  kwa  majina  ya  watu  maarufu  ili  kuwatapeli  watu.

0 comments:

Post a Comment